Home
Karibu Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo
Wasanii watakiwa kuzijua Sheria za Filamu na Michezo ya Kuigiza
 

Wasanii wa Filamu na Michezo ya Kuigiza wameshauriwa kuzisoma nyaraka mbalimbali za Bodi ya Filamu ili wajue sheria na kanuni zinazohusu tasnia hiyo.

Hayo yamesemwa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Joyce Fissoo alipokuwa akitoa ufafanuzi juu ya Sheria namba 4 ya Utengenezaji wa Filamu na Michezo ya Kuigiza ya mwaka 1976.

Read more...
 
Serikali ya China yaishukuru Tanzania kwa ushirikiano

 

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema kuwa Tanzania inafurahia uhusiano ulipo kati yake na China hususan katika tasnia ya Utamaduni.

   

Waziri Nchimbi ameyasema hayo jana jijini Dar es salaam wakati akiongea na kikundi cha sanaa cha Tianjin kilichotoka nchini China kushirikiana na jamii ya kichina inayoishi nchini kusherehekea mwaka mpya wa Kichina ujulikanao kama ‘Spring Festival.’

Read more...
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Naibu Waziri wa Utamaduni  wa china Mhe. Madam Zhao Shaohua anatarajia kuwasili hapa nchini tarehe 27 Julai, 2011 kwa ziara ya kikazi na ataongozana na  ujumbe wa viongozi 8 kutoka Wizara na Asasi za Utamaduni nchini China.

Read more...
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


YAH: TAARIFA YA KUWA MWENGE WA UHURU KUTOFIKISHWA KATIKA KILELE CHA MLIMA KILIMANJARO TAREHE 09 DESEMBA, 2011

 

Ndugu wananchi, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, inachukua fursa hii kukanusha taarifa zinazoendelea kuchapishwa na gazeti la Dira ya Mtanzania kama zilivyotolewa kwenye gazeti lao toleo Na. 145 la Jumatatu Januari 2 – 4, 2012 na gazeti toleo Na. 146 la Alhamisi Januari 5 -8, 2012.

 

Katika matoleo hayo yote, Gazeti hili linadai kuwa, Mwenge wa Uhuru haukufikishwa kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro na kwamba Serikali imewadanganya wananchi.

 

Ukweli ni kwamba, Mwenge wa Uhuru ulifikishwa katika kilele cha Mlima Kilimanjaro kama ilivyoagizwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete tarehe 1 Desemba, 2011 wakati akiwakabidhi Mwenge huo wapandishaji wa Mwenge kileleni Kilimanjaro.

Read more...
 
Viongozi wafanye kazi kwa bidii-Mama Maria Nyerere

Mjane wa Hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere akielezea jambo wakati alipotembelewa na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara (katikati) pamoja na Viongozi Waandamizi wa Wizara nyumbani kwake Butiama Mkoani Mara. Ziara hiyo ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe za miaka 50 ya Uhuru wa Tanazania Bara kwa upande wa Wizara hii zinazoendelea Katika viwanja vya Joseph Kazurira Nyerere kijijini Butiama. Kushoto kwa Naibu Waziri ni Naibu Katibu Mkuu, Bi. Sihaba Nkinga na kulia kwake ni Diwani wa Kata ya Butiama Mhe. Peter Wanzagi.

 

MJANE wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, Mama Maria Nyerere amewataka Viongozi Serikalini kufanya kazi kwa bidii na maarifa ili kuharakisha mchakato wa maendeleo kwa wananchi wake.

 

Ameyasema hayo leo wakati alipokutana na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara na Viongozi waandamizi wa Wizara hiyo waliokwenda kumtembelea nyumbani kwake kijijini Butiama, mkoani Mara.

Read more...
 
«StartPrev12NextEnd»

Page 1 of 2
 

Who's Online

We have 4 guests online